MTUNZI: MAULID BIN SWALEH
SHAIRI: CORONA
Janga limeikumba dunia, hatimae tunatanga
Tuiombee dunia, liondoke hili janga
Corona itaondoka, turudi kwa rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Hakika ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Kwetu ndio fundisho, tumkumbuke rabbana
Humfaa ukumbusho, anayerudi kwa rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Allah kaleta janga, kuwafunza waja wake
Kutokana na janga, msaada kutoka kwake
Corona ni fundisho, mponaji ni rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Tufanye istighari, atusamehe mola wetu
Tuondoe zetu jeuri, tumsabihi mola wetu
Tufanye masahihisho, atunusuru rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Corona inatumaliza, mkingaji ni rabbana
Ibadani kujituliza, tukimlilia rabbana
Hakika ni fundisho, muondoshaji rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Barakoa tunajikinga, pia kunawa mikono
Allah ndio kinga, tuinue kwake mikono
Mtume ni fundisho, katuletea rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Ushauri tunapewa, wanatoa madaktari
Unaenea kwa hewa, maneno ya madaktari
Bado ni fundisho, kimbilio ni rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Facebook: Maulid Bin Swaleh
Instagram: Maulid Bin Swaleh
Twitter: Maulid Bin Swaleh
Youtube: Maulid Bin Swaleh
Gmail: maulidbinswaleh@gmail.com
Contact no: ๐น๐ฟ๐น๐ฟ๐น๐ฟ Tanzania +255 756 716 511
*****************MWISHO*****************