Shairi la Corona(Covid-19).

MTUNZI: MAULID BIN SWALEH
SHAIRI: CORONA

Janga limeikumba dunia, hatimae tunatanga
Tuiombee dunia, liondoke hili janga
Corona itaondoka, turudi kwa rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana

Hakika ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana
Kwetu ndio fundisho, tumkumbuke rabbana
Humfaa ukumbusho, anayerudi kwa rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana

Allah kaleta janga, kuwafunza waja wake
Kutokana na janga, msaada kutoka kwake
Corona ni fundisho, mponaji ni rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana

Tufanye istighari, atusamehe mola wetu
Tuondoe zetu jeuri, tumsabihi mola wetu
Tufanye masahihisho, atunusuru rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana

Corona inatumaliza, mkingaji ni rabbana
Ibadani kujituliza, tukimlilia rabbana
Hakika ni fundisho, muondoshaji rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana

Barakoa tunajikinga, pia kunawa mikono
Allah ndio kinga, tuinue kwake mikono
Mtume ni fundisho, katuletea rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana

Ushauri tunapewa, wanatoa madaktari
Unaenea kwa hewa, maneno ya madaktari
Bado ni fundisho, kimbilio ni rabbana
Corona ni ukumbusho, kutoka kwa rabbana

Facebook: Maulid Bin Swaleh

Instagram: Maulid Bin Swaleh

Twitter: Maulid Bin Swaleh

Youtube: Maulid Bin Swaleh

Gmail: maulidbinswaleh@gmail.com

Contact no: ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ Tanzania +255 756 716 511



*****************MWISHO*****************

No comments:

Post a Comment

Maulid Bin Swaleh

JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI

JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI โœ๏ธAbdillah Kitota., MMDSC. ูˆูŽู‡ูุฒู‘ููŠ ุฅูู„ูŽูŠู’ูƒู ุจูุฌูุฐู’ุนู ุงู„ู†ู‘ูŽุฎู’ู„ูŽุฉู ุชูุณูŽุงู‚ูุทู’ ุนูŽู„ูŽูŠู’ูƒู ุฑูุทูŽุจู‹ุง...