Karibu katika blog hii kwa kupata nasheed , qur an na vinginevyo vinavyohusu dini ya uislamu unaweza kupata video zetu kupitia channel yetu ya youtube ambayo ni Maulid Bin Swaleh pia usisahau kusubscribe yetu(Welcome in this blog to get qaswida , nasheed , qur an ,and others inside the islamic)
Kufunga siku ya tisa (9) na kumi (10) ni bora zaidi kuliko kufunga siku ya kumi (10) na ya kumi na moja (11)
صيام التاسع مع العاشر أفضل من صيام الحادي عشر مع العاشر.
*KUFUNGA (SIKU) YA TISA (9) NA KUMI (10) NI BORA ZAIDI KULIKO KUFUNGA SIKU YA KUMI (10) NA YA KUMI NA MOJA (11).*
للعلامة الإمام عبد العزيز بن عبد الله بن باز- رحمه الله-
*(Fatwa) ya Mwanachuoni Mkubwa 'Abdul-'Aziiz bin 'Abdullah bin Baaz-Allah amrahamu-*
السؤال:
*Suali: 🎤*
ما حكم صيام يوم عاشوراء، وهل الأفضل صيام اليوم الذي قبله أم اليوم الذي بعده أم يصومها جميعا أم يصوم يوم عاشوراء فقط ؟ نرجو توضيح ذلك جزاكم الله خيرا.
*Ni ipi hukumu ya kufunga 'Aashuraa, na je ni bora zaidi kufunga siku ambayo inayofuata au siku (moja) kabla yake au afunge (siku) zote au afunge 'Aashuraa peke yake?*
نرجو توضيح ذلك جزاكم الله خيرا.
*Tunataraji ufafanuzi wa hilo Allah awalipe kheri.*
الجواب:
*Jawabu: 📚*
صيام بوم عاشوراء سنة؛
*Kufunga siku ya kumi ya mwezi wa Muharram (mfungo nne) ni sunnah,*
لما ثبت في الأحاديث الصحيحة عن رسول الله- صلى الله عليه وسلم من الدلالة علــے ذلك،
*Kwa sababu ya hadithi sahihi sa mtume- swala na salamu zimfikie-zinazojulisha hilo,*
وأنه كان يوما تصومه اليهود،
*Na hakika hiyo (siku) ni siku (ambayo) Mayahudi walikuwa wakiifunga,*
لأن الله نجى فيه موسى وقومه وأهلك فرعون وقومه،
*Kwa sababu Allah alimuokoa (ndani ya siku hiyo) Musa na watu wake na alimwangamiza Firauni na watu wake,*
فصامه نبينا محمد - صلــے الله عليه وسلم شكرا لله، وأمر بصيامه،
*Basi akafunga nabii wetu Muhammad kwa kumshukuru Allah, na akaamrisha ifungwe,*
وشرع لنا أن نصوم يوما قبله أو يوما بعده،
*Na akatuwekea (kuwa) ni sunnah tufunge siku (moja) kabla yake au siku (moja) baada yake,*
وصوم التاسع مع مع العاشر أفضل،
*Na kufunga (siku) ya tisa na ya kumi ni bora zaidi,*
وإن صام العاشر مع الحادي عشر كفــے ذلك، لمخالفة اليهود،
*Na kama (mtu) akifunga siku ya kumi na ya kumi na moja hilo linatosha kwa ajili ya kwenda kinyume na Mayahudi,*
وإن صامهما جميعا مع العاشر فلا بأس؛
*Na kama atazifunga (siku) mbili zote (9+11) pamoja na siku ya kumi basi (hilo) halina ubaya,*
لما جاء في بعض الروايات:
*Kwa sababu ya (maneno) yaliyokuja katika baadhi ya riwaya (ambayo) ni:*
”صوموا يوما قبله ويوما بعده“
*“Fungeni siku (moja) kabla yake na siku (moja) baada yake”*
أما صومه وحده فيكره والله ولي التوفبق.
*Ama kuifunga ('Aashuraa) peke yake inachukiza, na Allah ndiye msimamizi wa taufiq.*
📚 المصدر: مجموع فتاوى ابن باز (404/15)
*[ Chanzo: Maj'mu'u fataawa ibn Baaz (15/404) ]*
*Mfasiri: Abuu Thurayyaa Ismail seiph Mbonde - Allah amuhifadhi*
Dar es salaam, Tanzania 🇹🇿
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Maulid Bin Swaleh
JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI
JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI ✍️Abdillah Kitota., MMDSC. وَهُزِّي إِلَيْكِ بِجِذْعِ النَّخْلَةِ تُسَاقِطْ عَلَيْكِ رُطَبًا...

-
Jaa'far Mponda-Miski ya roho
-
Karibu katika blog hii kwa kupata taarifa mbalimbali juu ya dini ya kiislamu kama vile ,nasheed,qur an,mawaidha na vinginevyo.
-
صيام التاسع مع العاشر أفضل من صيام الحادي عشر مع العاشر. *KUFUNGA (SIKU) YA TISA (9) NA KUMI (10) NI BORA ZAIDI KULIKO KUFUNGA SIKU YA...
-
Imekusanywa na: Ummu Iyyaad Haki za mume na mke zimedhihirishwa katika Qur-aan na Sunnah. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: ...
No comments:
Post a Comment