Kufunga siku ya tisa (9) na kumi (10) ni bora zaidi kuliko kufunga siku ya kumi (10) na ya kumi na moja (11)



​صيام التاسع مع العاشر أفضل من صيام الحادي عشر مع العاشر.​

*KUFUNGA (SIKU) YA TISA (9) NA KUMI (10) NI BORA ZAIDI KULIKO KUFUNGA SIKU YA KUMI (10) NA YA KUMI NA MOJA (11).*


للعلامة الإمام عبد العزيز بن عبد الله بن باز- رحمه الله-

*(Fatwa) ya Mwanachuoni Mkubwa 'Abdul-'Aziiz bin 'Abdullah bin Baaz-Allah amrahamu-*


السؤال:

*Suali: 🎤*


ما حكم صيام يوم عاشوراء، وهل الأفضل صيام اليوم الذي قبله أم اليوم الذي بعده أم يصومها جميعا أم يصوم يوم عاشوراء فقط ؟ نرجو توضيح ذلك جزاكم الله خيرا.

*​Ni ipi hukumu ya kufunga 'Aashuraa, na je ni bora zaidi kufunga siku ambayo inayofuata au siku (moja) kabla yake au afunge (siku) zote au afunge 'Aashuraa peke yake?​*


نرجو توضيح ذلك جزاكم الله خيرا.

*Tunataraji ufafanuzi wa hilo Allah awalipe kheri.​*


​ الجواب:​

*Jawabu:  📚*

صيام بوم عاشوراء سنة؛

*Kufunga siku ya kumi ya mwezi wa Muharram (mfungo nne) ni sunnah,*


 لما ثبت في الأحاديث الصحيحة عن رسول الله- صلى  الله عليه وسلم من الدلالة علــے ذلك،

*Kwa sababu ya hadithi sahihi sa mtume- swala na salamu zimfikie-zinazojulisha hilo,*


 وأنه كان يوما تصومه اليهود،

*Na hakika hiyo (siku) ni siku (ambayo) Mayahudi walikuwa wakiifunga,*


لأن الله نجى فيه موسى وقومه وأهلك فرعون وقومه،

*Kwa sababu Allah alimuokoa (ndani ya siku hiyo) Musa na watu wake na alimwangamiza Firauni na watu wake,*


 فصامه نبينا محمد - صلــے الله عليه وسلم شكرا لله، وأمر بصيامه،

*Basi akafunga nabii wetu Muhammad kwa kumshukuru Allah, na akaamrisha ifungwe,*


وشرع لنا أن نصوم يوما قبله أو يوما بعده،

*Na akatuwekea (kuwa) ni sunnah tufunge siku (moja) kabla yake au siku (moja) baada yake,*


 وصوم التاسع مع مع العاشر أفضل،

*Na kufunga (siku) ya tisa na ya kumi ni bora zaidi,*


 وإن صام العاشر مع الحادي عشر كفــے ذلك، لمخالفة اليهود،

*Na kama (mtu) akifunga siku ya kumi na ya kumi na moja hilo linatosha kwa ajili ya kwenda kinyume na Mayahudi,*


 وإن صامهما جميعا مع العاشر فلا بأس؛

*Na kama atazifunga (siku) mbili zote (9+11)  pamoja na siku ya kumi basi (hilo) halina ubaya,*


 لما جاء في بعض الروايات:

*Kwa sababu ya (maneno) yaliyokuja katika baadhi ya riwaya (ambayo) ni:*


 ”صوموا  يوما قبله ويوما بعده“

*“Fungeni siku (moja) kabla yake na siku (moja) baada yake”*


 أما صومه وحده فيكره والله ولي التوفبق.

*Ama kuifunga ('Aashuraa) peke yake inachukiza, na Allah ndiye msimamizi wa taufiq.​*


📚 المصدر: ​مجموع فتاوى ابن باز (404/15)

*[ Chanzo: Maj'mu'u fataawa ibn Baaz (15/404​) ]*

*Mfasiri: Abuu Thurayyaa Ismail seiph Mbonde - Allah amuhifadhi*
Dar es salaam, Tanzania 🇹🇿


No comments:

Post a Comment

Maulid Bin Swaleh

JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI

JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI ✍️Abdillah Kitota., MMDSC. وَهُزِّي إِلَيْكِ بِجِذْعِ النَّخْلَةِ تُسَاقِطْ عَلَيْكِ رُطَبًا...