Uoshe(usafishe) moyo wako na utwaharishe.


UOSHE (USAFISHE) MOYO WAKO NA UTWAHARISHE!

قال العلامة ابن عثيمين - رحمه الله تعالى.
Amesema mwanachuoni mkubwa Ibn 'Uthaumin -Allah amrahamu-


فتش قلبك يا أخي،
Uchunguze moyo wako ewe ndugu yangu,


 هل فيك رياء؟
Je, kwako kuna (tabia ya) kujionesha?


هل فيك كراهة للحق؟
Je, kwako kuna (tabia ya) kuichukia haki?


 هل فيك بغضاء للمؤمنين؟
Je, kwako kuna (tabia ya) kuwabughudhi waumini?


هل فيك حقد على المؤمنين؟
Je, kwako kuna (tabia ya) kuwahusudu waumini?


فإن غسيل القلب كل يوم،
Basi (tambua) kuuosha moyo kila siku,


 أهم من غسيل الثياب كل يوم،
Ni muhimu zaidi kuliko kuifua nguo kila siku,


 اغسل قلبك وطهره.
Uoshe (usafishe) moyo wako na utwaharishe.


📚  المصدر: اللقاء الشهري (75/2)
[ Chanzo: Alliqaau l-sshahriy (2/75) ]*
Maelezo kutoka kwa mfasiri- Allah amuhifadhi

Usafishe (uoshe) moyo wako na maradhi haya ya moyo ambayo ni maradhi mabaya sana,
maradhi kama hayo aliyoyataja sheikh ambayo mengine ni sababu ya kuvunjika mahusiano na undugu baina ya waislamu,

Huu ni usia mzito mno, kwa sababu tulio wengi sasa hivi tuna maradhi ya nyoyo!! Unaweza ukatuona tumevaa na kupendeza na tunanukia vizuri lakini nyoyo zetu zinanuka na kutoa harufu ya *hasuda, roho mbaya, chuki, mafundo ya moyo, kiburi, kujiona!!*

Kwa ajili hii utaona mizozo haiishi katika safu zetu, na itaendelea kuwepo kama hatutajisafisha nyoyo zetu. ni hatari kubwa muislamu akawa na moyo mchafu!!


( ۚ أُولَٰئِكَ الَّذِينَ لَمْ يُرِدِ اللَّهُ أَن يُطَهِّرَ قُلُوبَهُمْ ۚ لَهُمْ فِي الدُّنْيَا خِزْيٌ ۖ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ) المائدة: (٤١)

(Hao ndio ambao Allah hakutaka kuzitakasa nyoyo zao (na uchafu wa shirki na kufuru), Watakuwa na udhalili (fedhea) duniani, na akhera watakuwa na adhabu kubwa). [ Al-Maaida (41) ]

*Mfasiri: Abuu Thurayyaa Ismail seiph Mbonde - Allah amuhifadhi*
Dar es salaam, Tanzania 🇹🇿

No comments:

Post a Comment

Maulid Bin Swaleh

JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI

JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI ✍️Abdillah Kitota., MMDSC. وَهُزِّي إِلَيْكِ بِجِذْعِ النَّخْلَةِ تُسَاقِطْ عَلَيْكِ رُطَبًا...