Mtoto anapopiga chafya.


MTOTO ANAPO PIGA CHAFYA*🎤


قال الشيخ صالح بن فوزان الفوزان حفظه الله :
Amesema Sheikh Swaaleh fauzaan bin Fauzaan- Allah amhifadhi-

"أما الصغير إذا عطس فإنه ﻻ يشمت ولكن يدعو له بالبركة يقال:

Ama mtoto mdogo akipiga chafya hakika haombewi dua (kwa kuambiwa “yarhamuka Allah” lakini ataombewa dua ya Baraka ataambiwa:


 بارك الله فيك لأنه عطس طفل عند النبي صلى الله عليه وسلم فقال :

Baaraka Allahu fiika, kwakua alipiga chafya mtoto mbele ya mtume swallah Allahu Alaih wasalam Akasema Mtume:

 (بارك الله فيك)
(Baaraka Allahu fiika)

وأمر الطفل إذا عطس أن يحمد الله من باب التعليم."

*Na ama kumuamrisha mtoto anapo piga chafya amhimid Allah (aseme Alhamdulillah) ni katika mlango wa Kumfunza*


📚 المصدر: شرح منظومة الآداب الشرعية (ص٢٨٠)

[ Chanzo: Sharhu Man-ndhuumat Aadaab As-shar'iyyah (ukurasa wa 280) ]

Kwa maana hio watoto wetu khasa wale ambao hawajaanza kusema wakipiga Chafya tunawaambia “Baaraka Allahu fiika”
Ama wale ambao wameanza kuongea tutawaambia waseme “Alhamdulillah” na kisha nasi tutasema Yarhamuka Allah na kisha tutawaeleza waseme “yahdiikumu Allahu wayuslih Baalakum”.
Na Allah ndiye mjuzi zaidi

No comments:

Post a Comment

Maulid Bin Swaleh

JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI

JINSI ULAJI WA TENDE UNAVYOSAIDIA LEBA YA UZAZI ✍️Abdillah Kitota., MMDSC. وَهُزِّي إِلَيْكِ بِجِذْعِ النَّخْلَةِ تُسَاقِطْ عَلَيْكِ رُطَبًا...